
1985 - 2007
2. Habari Njema
Support Pages
Index To All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
Soma Haya Katika Biblia Yako
1 Wakorintho 15:1-34; 15:58
Mstari wa Kukariri
“Kwa maana siionei haya injili, kwa
sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu, kwa kila aaminiye…” Warumi
1:16.
Baadaye Tafakari Kuhusu Jambo Hili
Je, umeshatubu dhambi zako na kumpokea
Yesu kuwa Mwokozi wako? Ikiwa bado, huu ndio wakati mwafaka wa kufanya hivyo.
Jambo la Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Jiamulie mwenyewe ni wasioamini wangapi
utakaowapelekea habari hizo kuu. Je ni mmoja, wawili, wanne au zaidi?
Usivuke kiwango cha imani yako, lakini weka lengo na umwombe Mungu akuwezeshe.
Kazi ya Kuandika ya Stashahada
Andaa mahubiri ya kurasa mbili kuhusu
somo utakalochagua mwenyewe, lakini pia uhusishe vipengele vya maarifa
uliyoyapata kutokana na somo hili la Injili.
Tafakari Mistari Ifuatayo, Neno Kwa Neno
Mithali 30:2-4
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea Taifa La Mauritania
Idadi ya Watu ni 2,500,000
Watu Wasiomjua Yesu ni 99.7%
Hakikisha umewafundisha wengine somo hili.
Kila mara
omba na kujiandaa ukiongezea mistari mingine ya Biblia
na mifano yako mwenyewe
ili kufanya somo lieleweke vizuri zaidi.
(1) Je, Waweza Kusikia Swali?
Je, waweza kusikia rohoni mwako kilio cha moyo mtulivu
ukiulilia ulimwengu wa vatu? Hebu sikiliza.
Nimechoka ee
Mungu
Nimechoka ee
Mungu, na kuzimia
Mimi ni mjinga
kuliko watu wote
Sina ufahamu wa
kibinadamu
Sijajifunza
hekima, wala sina maarifa kumhusu Yeye Aliye Mtakatifu
Je, ni nani
aliyepaa mbinguni na kushuka tena chini?
Je, ni nani
aliyeukusanya upepo mikononi mwake?
Je, ni nani
aliyeyafungia maji katika vazi lake?
Na je, ni nani
aliyefanya imara miisho yote ya dunia?
Jina lake ni nani?
Na mwanaye jina lake nani?
Niambie kama unajua!
(Mit 30:1-4)
Mamilioni ya
watu wamechanganyikiwa kwa kutokujua maana halisi ya maisha. Hawajui
walikotokea, ni kwa nini wapo hapa, na ni wapi watakwenda maisha yanapofikia
ukomo. Mioyoni mwao wanahisi yupo Mungu, lakini ni nani huyo Mungu, anakaa
wapi, na anafananaje? Wewe unamfahamu huyo Mungu, na jina la Mwanaye unalijua,
ni Bwana wetu Yesu Kristo.
(2) Tumwambie Nini?
Katika kujibu swali hilo, Paulo aliwaandikia rafiki zake
kwenye kanisa lililokuwa Korintho huko Ugiriki. Alisema kuna mambo sita muhimu
ambayo watu wanapaswa kuyajua ili waweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu lile
watakalo kulifanya
(1Kor 15:1-28).
o
Kuna ujumbe kutoka kwa Mungu
o
Yesu aliyekufa, amefufuka na yu hai
o
Kuna neema na fadhila kutoka kwa Mungu
o
Kifo si mwisho
o
Yesu Kristo anakuja tena
o
Kutakuwa na siku ya mwisho
(3) Mwambie Anaweza Kumjua
Mungu
Biblia inasema kuwa, “ ni jambo la umuhimu wa kwanza”
kwamba kila mtu, awe mwanamume au mwanamke, mvulana au msichana, kila mtu
aisikie Injili, ambayo ni ujumbe unaomwunganisha tena mwanadamu na Mungu.
Je, Hiyo Injili Ni Nini?
Ni uweza wa
Mungu kwa kila aaminiye (Rum 1:16). Paulo anatuambia kwamba Kristo, mwana wa
Mungu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, akazikwa, na siku ya tatu akafufuka
(1Kor 15:1-4).
1. Lazima
tuamini kwamba Mungu yupo, na Yeye ndiye anayewakirimia wote wamtafutao kwa
bidii. Yeye si katili, wala hayupo mbali (Ebr 11:6).
2.
Ni lazima tuamini kwamba Yeye ni Mungu Mtakatifu, na ya
kwamba dhambi zetu nyingi; za kutokumtafuta Yeye, na kujiendea njia zetu
wenyewe, mawazo mabaya, maneno mabaya na matendo mabaya; zote hizo
zimetutenganisha sisi mbali na upendo wa Mungu na uwepo wake. Matokeo yake ni
kwamba baada ya kifo ni adhabu ya kutisha ( Rum 3:23; 6:23).
3.
Tunachagua kuamini kwamba Mungu katika upendo wake mkuu
alimtuma Mwanaye Yesu, akazaliwa na bikira, katika hali ya kutokuwa na dhambi,
ili atunusuru kwa kuichukua asirá ya haki ya Mungu, ili kwamba tuweze kuwa na
amani na Mungu, na pia tuweze kupaingia patakatifu pake sasa na katika kufa
kwetu (1Pet 2:24,25).
4.
Tunaamini kuwa ni wajibu wetu kufanya mwitikio sahihi.
Tunakubali kwamba tumetenda dhambi na kwa kweli tunajuta sana kwa hali hiyo.
Tunaamini kwamba Yesu alikufa kwa ajili yetu, na sasa tunamwomba Mungu
atuwezeshe kuacha uovu. Tunampokea Yesu kuwa Mwokozi na Bwana, na kuahidi
kumfuata Yeye situ zote hata kama rafiki na jamaa wataleta shida (Yn 1:12,13)
(Ufu 3:20).
(4) Mwambie Kwamba Yesu Yu
Hai
Imani yetu haikujengwa juu ya hisia tu, bali imesimama
kwenye kweli zinazoweza kukubalika na mahakama yo yote kama vielelezo muhimu
vya ushahidi. Paulo anaandika ushuhuda wa watu
514 ambao walishuhudia kwa macho yao; ambao ni pamoja na wale waliotoa taarifa
za Yeso kwa sababu walimfahamu vizuri. Hao ni kama Petro na wale mitume
wengine, ambao kwa vyo vyote wasingeweza kufanya mañosa katika kumtambua Bwana
(1Kor 15:5-8).
(5) Mwambie Kwamba Neema Ipo
Kwa Ajili Yake
Neema ni haki asiyostahili mtu, anayoipokea bure kutoka kwa
Mungu. Hainunuliwi wala haipatikani kwa malipo; inapokelewa tu kwa shukrani.
Paulo anasema, ingawa alilitesa kanisa, hata hivyo neema ya Mungu imefanya kazi
kwa nguvu maishani mwake. Neema ya Mungu ilimwinua Paulo kutoka katika kuwa
mkuu wa wenye dhambi, na kuwa mtu wa Mungu mwenye uwezo mkubwa (1Kor 15:9,10).
(6) Mwambie Kwamba Kifo Si
Mwisho
Ni hapo tu tutakapokuwa tumemchagua kumfuata Yesu, Edipo
hapo tutakapoweza kuingia katika uwepo wa Bwana situ ya kufa kwetu.
Tunatarajia ufufuo ujao ambapo waamini watavikwa miili mipya isiyozeeka,
isiyougua wala kufa. Tutaishi kwenye dunia mpya na chini ya mbingu mpya. Lakini
wasioamini watarajie tu ziwa la moto na mateso yasiyokoma mbali na upendo wa
Mungu (1 Kor 15:12-23, 35-49).
(7) Mwambie Yesu Anakaribia
Kurudi
Atakapokuja ataleta haki kwa watu wote hapa duniani,
tukiamini ahadi ya malaika katika Matendo 1:11, na ya wakristo wa vizazi vyote
hadi kufikia leo (1 Kor 15:23,25).
(8) Mwambie Kwamba Kuna Siku
Ya Mwisho
Leo ndiyo siku ya kupokea wokovu wa Mungu; na sasa ndiyo
wakati mzuri zaidi maana kwa kesho huenda ukawa umeshachelewa (1 Kor 15:24-28,
50-57). Kwa sababu hizo, sisi tulioamini tusimame imara, na kukataa kuondoshwa
kwenye hizo kweli za milele. Tunapaswa kujitoa kikamilifu kwa kazi ya bwana, na
kuwaambia wengine, tukijua kwamba ingawa kazi yenyewe ni ngumu, lakini
haitakuwa bure (1Kor 15:58).
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili ya Watu wa
Ulimwengu
Huu Ambao Bado Hawajafikiwa na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
|
Afghanistan
|
|
Majina Yao
|
Lugha Zao
|
Idadi
Yao
|
|
Aimaq, Jamshidi (Char
Aimaq)
|
Aimaq, Jamshidi
|
92,000
|
|
Aimaq, Timuri (Teymur,
Timuri)
|
Aimaq, Taimuri
|
104,000
|
|
Darwazi (Badakhshani)
|
Darwazi
|
10,000
|
|
Gawar-Bati (Narisati)
|
Gawar-Bati
|
10,000
|
|
Munji-Yidgha
|
Munji
|
10,000
|

1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
for this revision and translation from the original English
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide
copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial
purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index To All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index