1985 - 2007


4. Dondoo Za Maandalizi Ya Wokovu

Watu Unaokutana Nao Wanaweza Kuokolewa

Support Pages   Index To All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index


Kwenye Biblia Yako Soma
1 Pet 3: 8 -22; Dan 12: 2-4

Mstari Wa Kukariri
Mwe tayari sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu;
lakini kwa upole na kwa hofu (1 Pet 3:15)

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, ni maswali gani unayoweza kumwuliza mtu na majibu yake yakakupa wewe fursa ya kumshuhudia mtu huyo?

Mambo Ya Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Hebu fikiri na ukumbuke jinsi Bwana mwenyewe alivyokuongoza katika  kumwamini, na jinsi alivyokusaidia baada ya kumwamini. Hebu yaandike hayo  mahali na kisha ufanye mazoezi ya kuwasimulia rafiki zako mpaka uweze kufanya hivyo katika hali ya utulivu, isiyo ya kidini, kwa muda wa dakika mbili.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika taarifa ya kurasa mbili kuhusu ule mfano wa mwana mpotevu na jinsi unavyojifunza kuhusu watu waliopotea na mpango wa Mungu wa kuwaokoa.

Tafakari Mstari wa Biblia Ufuatao Neno Kwa Neno
2 Tim 1:7

Tumia Muda wa Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Ubelgiji
Wako Wazungu10,000,000;  Ni Makao Makuu ya Umoja wa Ulaya;
Ni nchi yenye viwanda vingi; Wakristo waliopo ni 0.32% tu (Makanisa ya Kiinjili)

 

 

Hakikisha umewafundisha wengine somo hili.
Kila mara omba na kujiandaa ukiongezea mistari mingine ya Biblia
na mifano yako mwenyewe ili kufanya somo lieleweke vizuri zaidi.
 



Petro, Mtume mkuu na Mchungaji mpendwa amefanya pia kazi za Mwinjilisti mara kwa mara. Katika 1Pet 3:1-8 anaufungua moyo wake kama mchungaji, lakini katika mstari wa 13 anawatia moyo washirika wake katika huduma ya ushuhudiaji. Tunaenda kufuata mawaidha yake mema.

1. Ni Lazima Tuishinde Hofu

Katika nchi ya Hispania lipo kanisa la watu ambao awali waliishi mitaani. Watu hawa walikuwa wakiibia watu wengine, walitumia madawa ya kulevya na kufanya ukahaba, bila hofu yo yote. Yesu,kwa njia ya ajabu, amewaokoa kwa mamia. Walizoea kuiba hata kwenye mabenki; lakini baada ya kuokoka ukiwaambia habari ya kwenda kuwashuhudia watu wengine habari za Yesu ni ajabu kwamba wanaogopa, na kuja na hoja kama:

" Watu wanaweza kunicheka."

" Watu wanaweza kufikiria mimi nimekuwa mwendawazimu."

" Mtu anaweza kunipiga halafu. "

" Mimi sitaki kujisikia kukataliwa ujue."

Biblia inasema kwamba Mungu hakutupa sisi roho ya woga, bali roho ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi (2Tim 1:7)

Sasa Hii Hofu Inatoka Wapi?
Je, ni nani asiyetaka sisi kuwajulisha watu habari za Yesu? Ni Shetani. Ikiwa tutanyenyekea mbele za Mungu, tutaweza kumpinga Shetani naye atatukimbia (Yak 4:7).

2. Ni Lazima Tukae Sawa Mioyoni Mwetu!

Ndani ya mioyo yetu ni lazima tumkubali Kristo kuwa Bwana. Kuwa chini ya Ubwana maana yake ni kuyafanya mapenzi yake; maana yake ni kufanya  kila analosema ni muhimu kwake. Je, mapenzi ya Bwana wetu Yesu Kristo ni yapi?

  1. Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea (Lk 19:10).

  2. Roho wa Bwana yu juu yangu, amenipaka mafuta ili niwahubirie maskini habari njema (Lk 4:18).

  3. Je, hawaachi wale tisini na tisa na kwenda kumtafuta yule kondoo mmoja aliyepotea hadi ampate? (Lk 15:4).

Watu waliopotea na wale waliochanganyikiwa, hao ndio walio muhimu kwa Yesu. Ni kweli mtu anaweza kuponywa kutoka kwenye kitanda cha mauti, lakini ni bora zaidi kijana anapomfuata Kristo akaponywa mwili na nafsi pia. Nani ajuaye ni wangapi wanaoweza kumfuata Yesu baada yake?

3. Petro Anasema, ‘Kila Mara!’

Ni lazima tuwe tayari kuzungumza habari za Yesu wakati wote mchana na usiku. Unaweza kuwa na uhakika  kwamba Mungu anaweza kuandaa mpango wa kukujaribu ili ajue uaminifu wako. 

Mahali fulani kule India kikundi fulani cha wakristo waliokuwa wamechoka sana baada ya kazi ngumu katika mazingira ya joto na vumbi, walikaa kwenye mghahawa mmoja ili kujipatia riziki. Mara akatokea mhudumu Mhindu na kuanguka miguuni pao na kusema anawajua wao ni akina nani; na kisha kuwaomba wamsaidie ili aweze kumpokea Yesu. Huu haukuwa muda mzuri kwao, lakini unadhani walifanya nini? Kila mara!

4. Je, Umejiandaa?

Petro anasema ni lazima tujiandae kabla hatujaingia kwenye mapambano la sivyo ipo hatari ya kushindwa. Je, tunapaswa kujiandaa kwa namna gani? Jiandae kwa namna zifuatazo ~

5. Petro Anatumia Neno Hili, ‘Kila Mmoja!’

Wakati mwingine tunapata urahisi wa kuishi na baadhi ya watu, lakini tunapata ugumu kuishi na wengine. Lakini linapokuja suala la kushuhudia tunapaswa kuweka kando kila aina ya ubaguzi na upendeleo, kwa sababu kwa Yesu kila nafsi ni ya thamani; iwe ni ya mkubwa, ya mfanyakazi, au ya mtu wa hali ya chini. Mungu anapenda nafsi zote sawasawa.

6. Waruhusu Wakuulize Maswali!

Je, waweza kuanzisha mazungumzo yatakayomfanya mtu akuulize, kwa mfano, unafanya nini au kwenda wapi miisho ya wiki? Kuulizwa swali kama hilo kunakupa wewe fursa nzuri ya kusema maneno machache kuhusu imani yako au kanisa lako. Mkakati uliopo ni kuvua watu, na kumvua samaki ni lazima utumie ndoano yenye chambo.  Angalia yule unayeweza kumkamata kwa uvumilivu, na huku jicho lako likiwa wazi kuona fursa zingine anazoweza kukupa Mungu.

Fursa Zaweza Kujitokeza Bila Kutazamiwa

Mchungaji mmoja aliyekuwa anasafiri kwa treni alikaa jirani na msichana ambaye baadaye alishambuliwa na pumu. Abiria wote walitazama pembeni, lakini Mchungaji yule alimwendea msichana na kumtuliza. Akasema anajua jinsi msichana huyo anavyojisikia kwa sababu yeye mwenyewe aliwahi kuugua pumu. Baadaye yule msichana alitaka kujua ni kwanini sasa haugui tena pumu. Kwa dakika chache Mchungaji yule aliweza kuelezea imani yake aliyonayo kwa Mungu anayeponya. Msichana huyo aliahidi kumtembelea Mchungaji yule.

7. Je, Unaweza Kueleza Tumaini Ulilonalo?

Unapokuwa ukizungumza na mtu mtaani na mazungumzo yenu yakabadilika na kulenga kwenye imani katika Mungu, bila shaka hutachukua zaidi ya dakika mbili kumweleza ni nini Yesu alichokufanyia. Je unaweza kufanya hivyo? Kwanini usifanye mazoezi na rafiki zako? Kila mmoja atafanya zoezi la kumshuhudia mwenzake kwa zamu.

8. Chunga Sana Msimamo Wako

Msimamo wako na tabasamu lako vyaweza kusema kwa sauti kubwa kuliko maneno. Petro anasema kwamba tunapaswa kusema kwa upole na adabu. Sifa hizi ni adimu sana katika ulimwengu tunamoishi sasa.

9. Hatimaye Uwe Tayari Kuteseka

Petro anasema kwamba, ikiwa ni mapenzi ya Mungu, uwe tayari kuteseka kwa kufanya mema. Baadhi ya watu hawatataka kukusikiliza. Usijali hata kama watakucheka au kukutukana. Yote ni juu ya Yesu aliyefia dhambi mara moja tu,mwenye haki kwa ajili ya wasio haki; huyo atakuleta kwa Mungu. 


Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu
Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili; Wataje Kwa Majina
 

Algeria

Jina La Watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Hoggar, Ahaggaren

Tamahaq, Hoggar

31,000

 

 


 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
for this revision and translation from the original English
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index To All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index